Alhamisi, 16 Julai 2015

Kuganda kwa Asali


        
Kuganda kwa asali ni tabia ya asali kubadilika na kutengeneza chengachenga. Tabia hii inatokana na viundo vya asali na namna ilivyohifadhiwa. Aina nyingine ya asali haigandi wakati nyingine huganda mara tu baada ya kukamuliwa au hata ikiwa bado kwenye masega. Aina kuu mbili za sukari zilizomo kwenye asali (fruktosi na glukosi) ndizo zinazosababisha kuganda kwa asali. Kadiri kiwango cha glukosi kinavyoongezeka ndivyo asali inavyoganda kwa haraka na kiwango kikubwa cha fruktosi huchelewesha kuganda kwa asali. Vitu vingine vinavyosababisha kuganda kwa asali ni kushuka kwa joto, asali kuwa na ukungu na aina ya mimea.

Hakuna maoni: